Alhamisi , 12th Jun , 2025

Trent Alexander Arnold ametambulishwa rasmi ndani ya kikosi cha Real Madrid na kukabidhiwa jezi namba 12 aliyokuwa akivaa mbrazil Marcelo aliyeondoka klabuni hapo 2022 na kutimkia Olympiacos.

Trent Alexander Arnold

Muingereza huyo mwenye umri wa miaka 26 alipokuwa Liverpool alikuwa anavaa jezi namba 66 aliyokuwa akivaa katika timu za vijana lakini amelazamika kubadili namba ya jezi kutokana na sheria za Laliga kukataza mchezaji kuvaa jezi yenye namba zaidi ya  25.

Beki huyo wa kulia alisema rekodi ya washindi mara 15 wa kombe la Ulaya ilibidi "iheshimiwe" na alitaka kuiongeza.

"Sababu kubwa iliyonifanya nijiunge ni kuwa sehemu ya historia ya ajabu ambayo klabu ina," alisema.Kuwa sehemu ya mafanikio kwenda mbele, jiunge na timu ya kusisimua, changa yenye uwezo mkubwa."

Alexander-Arnold, ambaye alihamia kwa ada ingawa kandarasi yake ilikuwa inaisha msimu huu wa joto, ili kuharakisha kuwasili kwake kabla ya Kombe la Dunia la Klabu, alisaini mkataba hadi 2031.