Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ushindi wa Simba SC wabeba ujumbe wa Balozi 2020

Jumatatu , 30th Nov , 2020

Balozi wa Tanzania nchini Nigeria, Dkt. Benson Bana amesema ushindi wa Simba SC dhidi ya Plateau United ni ushindi wa taifa kwa ujumla na mwaka 2020 kwa Tanzania ni mwaka wa ushindi.

Balozi wa Tanzania nchini Nigeria Benson Bana ( wa kwanza kushoto) akiwa na viongozi wa Simba SC.

Balozi Bana ameeleza hayo jana usiku baada ya mchezo wa kwanza hatua ya awali Ligi ya Mabingwa Afrika, ambapo Simba SC ilishinda 0-1 dhidi ya Plateau United.

"Ushindi wa leo ni ushindi wa Watanzania. Vijana wamefanya kile kilichotarajiwa na Watanzania, na sasa tujipange kwaajili ya mchezo wa marudiano na mwaka 2020 kwa Tanzania ni mwaka wa ushindi."- Balozi wa Tanzania nchini Nigeria, Dkt. Benson Bana.

Kwa upande wake kocha wa Simba Sven Vandenbroeck amesema, "Ulikuwa mchezo mgumu, wana nguvu na walijaribu kiufundi kutafuta goli lakini nawapongeza wachezaji wangu sababu dakika zote 90 walikuwa wanakimbia kuzuia. Nafikiri tunatakiwa kuwa na furaha sana na ushindi. Matokeo mazuri lakini bado hatujamaliza sababu wiki ijayo tuna dakika 90 zingine".

Benchi la ufundi la Simba SC chini ya kocha mkuu Sven Vandenbroeck (katikati).

Simba SC imeanza safari ya kurejea Tanzania alfajiri ya leo Novemba 30, 2020 na inatarajiwa kutua kesho Jumanne Saa 10:00 jioni, kwenye uwanja wa ndege wa Kilimanjaro.

Mchezo wa marudiano utapigwa Desemba 5, 2020 kwenye uwanja wa Mkapa jijini Dar es salaam, ambapo Simba SC inahitaji sare ya aina yoyote ili kusonga mbele.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali