Jumanne , 20th Mei , 2025

Mmiliki mwenza wa Manchester United Sir Jim Ratcliffe ameshuhudia utajiri wake ukishuka kwa £6.473bn  ikiwa ni zaidi ya robo ya utajiri wake katika kipindi cha  mwaka mmoja uliopita  kwa mujibu wa orodha  ya hivi punde iliyotolewa  na   Sunday Times.

Sir Jim Ratcliffe - Mmiliki mwenza wa Manchester United

Sir Jim mwenye umri wa miaka 72 utajiri wake umepungua kutoka £23.519bn hadi £17.046bn na kumfanya ashuke  kutoka nafasi ya nne hadi ya saba kwenye orodha ya kila mwaka ya watu 350 matajiri zaidi nchini Uingereza.

Kundi la Ineos la Ratcliffe lilinunua hisa za asilimia  27.7 katika klabu ya Manchester  United mwezi Februari 2024 kwa mkataba wa thamani ya takriban £1.25bn ($1.6bn) na kupata mamlaka ya kuimiliki klabu hiyo kubwa nchini England 

Ikumbukwe wafuasi wengi wa Manchester United wanakosoa uwepo wa bilionea huyo tangu ajiunge na klabu hiyo baada ya United kupandisha bei ya tiketi na kupunguza wafanyakazi katika jitihada za kuboresha kitengo cha fedha katika klabu hiyo