Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Vita ya Simba na Yanga kwa mchezaji, wakala aeleza

Jumatano , 27th Mei , 2020

Klabu za Simba na Yanga ziko katika vita ya kuwania saini ya mlinzi matata wa klabu ya Coastal Union, Bakari Nondo Mwamnyeto kuelekea msimu ujao wa 2020/21.

Haruna Niyonzima wa Yanga, Luis Miquissone na Meddie Kagere wa Simba

Beki huyo amekuwa katika midomo ya wadau wengi wa soka msimu huu kutokana na umahiri wake wa kuzuia na kuisaidia klabu ya Coastal Union kufikia katika nafasi nzuri msimu huu.

Wakala wa mchezaji huyo ambaye pia ni mchezaji wa zamani wa soka katika mkoa wa Tanga, Kasa Mussa amethibitisha mchezaji huyo kuhitajika na klabu hizo kubwa nchini na kwamba kinachosubiriwa ni msimu kumalizika ili waweze kukamilisha dili na moja ya klabu hizo.

Amesema kuwa Yanga wameonesha nia ya kumuhitaji pamoja na Simba lakini mpaka sasa hajafikia makubaliano ya dau la uhamisho na klabu ya Yanga ambao ndio wako katika mazungumzo mazuri.

Klabu ya Yanga imesharejea mazoezini jana baada ya kukamilisha vipimo vya wachezaji na benchi la ufundi, hivyo leo mazoezi rasmi yanatarajia kuanza sambamba na Simba na Azam FC ambao wanatarajia pia kuanza mazoezi yao leo.

Pia Serikali kupitia Baraza la Michezo Tanzania BMT inatarajia kutoa mwongozo rasmi kuelekea kurejea kwa Ligi Kuu Tanzania Bara na Ligi Daraja la Kwanza na la Pili, ikiwemo suala la mwongozo wa afya.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi