Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Vita ya nusu fainali yajulikana

Jumatatu , 23rd Jul , 2018

Droo ya mechi za nusu fainali ya Sprite Bball Kings imefanyika usiku  wa Julai 23, kwenye ofisi za East Africa Television na kurushwa moja kwa moja kupitia kipindi cha '5Sports' na kusikika kupitia 'The Cruise' ambapo mabingwa watetezi Mchenga Bball Stars watakutana na Portland.

Manahodha wa timu 4 zilizopo hatua ya nusu fainali.

Katika mechi hiyo timu ya Portland itakuwa ndio timu mwenyeji kwenye nusu fainali ambayo itakuwa na jumla ya mechi tatu 'Best of three' lakini ikitokea timu moja imeshinda mechi mbili mfululizo, inakuwa imetinga fainali moja kwa moja hivyo mechi ya tatu haitakuwepo. Endapo kila timu itashinda mechi moja kati ya hizo mbili italazimika kuchezwa mechi ya tatu ili kuamua nani anakwenda fainali.

Droo hiyo pia imezikutanisha timu za Flying Dribblers ambao watakuwa wenyeji wa Team Kiza kwenye nusu fainali nyingine ambayo nayo itachezwa kwa mtindo huo huo wa mechi tatu ambazo zitafikiwa endapo timu hizo zitagawana ushindi kwenye mechi mbili za kwanza.

Mechi hizo za kwanza kwenye nusu fainali hiyo zitapigwa Jumamosi Julai 28, 2018 na mechi za pili zitapigwa Jumatano Agosti 1. Viwanja ambavyo vitatumika vitatangazwa hivi karibuni endelea kukaa karibu na East Africa Television na East Africa Radio.

Katika mechi za robo fainali Mchenga walishinda pointi 84 dhidi ya 67 za St. Joseph huku Portland wakiitoa Temeke Heroes kwa vikapu 84 dhidi ya 70. Flying Dribblers wao waliwatoa Water Institute kwa pointi 100 dhidi ya 64. Team Kiza waliiadhibu DMI kwa pointi 82 kwa 47.

Bingwa wa mashindano haya yanayodhaminiwa na kinywaji baridi cha Sprite, atajinyakulia kitita cha shilingi milioni 10 huku mshindi wa pili akitwaa milioni 3 na mchezaji bora wa mashindano 'MVP' akiondoka na shilingi milioni 2.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi