Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wachezaji 6 Simba walioumia warejea kikosini

Jumanne , 12th Oct , 2021

Wachezaji sita wa kikosi cha kwanza cha Simba waliopata majeraha wiki mbili zilizopita wamepona na wameanza mazoezi ya pamoja ili wacheze dhidi ya Jwaneng Galaxy ya Botswana kuwania kufuzu makundi Klabu bingwa Afrika.

Wacheza wa Simba wakiwa kwenye mazoezi ya pamoja.

Wachezaji hao ni mlinzi wa kati Joash Onyango na kiungo Sadio Kanoute, Onyango aliumia kichwani wakati Kanoute aliumia mguu kwenye mchezo wa fainali ya Ngao ya Hisani ya Jamii dhidi ya Yanga Septemba 25, 2021.

Onyango yupo fiti kwani alijumuishwa kwenye kikosi cha timuya taifa ya Kenya kwenye michezo miwili ya kuwania kufuzu kombe la Dunia dhidi ya Mali na Rwanda wakati Kanoute alisalia nchini kufanya mazoezi na kambi ya Simba.

Mlinzi wa kulia aliyeumia kwenye mchezo dhidi yaBiashara United Mara Septemba 28, 2021, Shomari Kapombe na Erasto Nyoni aliyeumia mazoezi wawili hawa nao wamerejea kikosini na wamefanya mazoezi na wenzao.

Wachezaji wengine ambao wamerejea kwenye utimamu wao ni mlinzi wa kati Kennedy Juma na winga Pape Ousmane Sakho ambao walioumia wote kwenye mchezo wa Simba dhidi ya Dodoma Jiji Oktoba 1, 2021 na kushindwa kuendelea na mchezo huo.

Kennedy Juma aliyepigwa kiwiko na mchezaji wa Dodoma Jiji, Anuary Jabir, aliitwa kwenye mchezo wa Taifa Stars dhidi ya Benin  Oktoba 10, 2021 na kuonesha kiwango safi huku Sakho alisalia na kambi ya Simba tokea wiki iliyopita.

Kurejea kwa wachezaji hao pamoja na mshambuliaji wa Kibu Denis kupata vibali vya kuchezea Simba akiwa raia wa Tanzania, vitawafanya wekundu hao wa msimbazi wawe na machaguo mengi kuwavaa Galaxy Jumapili ya Oktoba 17, 2021 kuwania kufuzu hatua ya makundi michuano ya klabu bingwa Afrika

 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali