Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Walichozungumza makocha na manahodha Simba, Yanga

Ijumaa , 3rd Jan , 2020

Kuelekea mchezo wa 'Watani wa Jadi' Simba na Yanga kesho Januari 4, leo umefanyika mkutano wa makocha pamoja na manahodha wa timu zote mbili kuelezea maandalizi yao.

Mkutano wa Simba, Yanga na wanahabari kuelekea mechi yao

Vifuatavyo ni baadhi ya vitu muhimu walivyovizungumza kuelekea kwenye mchezo huo.

Kocha wa Simba, Sven Vanderbroeck amesema, "tumecheza mechi nne ndani ya siku 10 na tumeshinda zote, tunajua kuna hisia fulani unaweza kujihisi ni bora lakini hii ni derby na ina ugumu wake, ina hisia zake. Mitandaoni joto ni kubwa sana na kuna wanaosafiri mbali kuja kuitazama mechi hii pekee, hivyo tunajiandaa. Kikosi changu kipo vizuri isipokuwa Rashid Juma ambaye atakuwa nje wiki kadhaa lakini wengine wote wako fiti", amesema Sven.

Kocha wa Yanga, Boniface Mkwasa

"Tumetoka kwenye ratiba ngumu ya mechi lakini nashukuru tumepambana japo tumepata majeraha. Tumejiandaa vizuri kwa mchezo, kama wao wameshinda mechi nne tano basi na sisi tutakuwa wa kwanza kuwafunga", amesema Mkwasa.

"Tunawaheshimu Simba na katika mpira kila mmoja anajiandaa. Tunawaheshimu na wana uongozi na wachezaji wazuri lakini uwanjani maamuzi ni dakika 90. Tunawaomba waamuzi wachezeshe kwa uhalali bila shinikizo lolote", ameongeza.

Kuhusiana na majeraha ya timu yake, kocha Mkwasa amesema, "tutawakosa wachezaji wawili, Lamine Moro ambaye ana kadi tatu za njano na Tariq Seif ambaye aliumia katika mechi ya mwisho lakini wengine wote wako vizuri. Kila mchezaji wetu anataka kucheza hii mechi hata kama ni leo

Nahodha wa Simba, John Bocco amezungumzia kwa upande wao jinsi walivyojiandaa, "wachezaji tumejiandaa vizuri, tunajua ubora wa Yanga wana kocha na wachezaji wazuri. Tunaamini tutapata ushindi kesho kutokana na maandalizi tuliyopewa na kocha, pia matokeo ya mechi zetu hivi karibuni yanatupa morali

Naye nahodha wa Yanga, Juma Abdul kwa niaba ya wachezaji wenzake, amesema, "nawaomba mashabiki wetu wa Yanga wasiogope kitu wajitokeze kwa wingi kesho wakijiamini kwa sababu tumejiandaa kushinda. Mashabiki wa Simba wasije uwanjani na matokeo yao, yoyote aliyejipanga anataondoka na pointi tatu".

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi