Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wenger aingilia kati kichapo cha Man United 

Jumatano , 13th Feb , 2019

Kocha wa zamani wa Arsenal, Arsene Wenger amesema kuwa kitu kikubwa kilichopelekea Manchester United kufungwa katika mchezo wa Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya PSG ni kutokana na kutomiliki mpira.

Kocha Arsene Wenger na wachezaji wa PSG na Man United

Wenger amesema hayo alipokuwa akifanya uchambuzi na kituo cha beIN SPORTS, ambapo amesema timu inapokuwa mwenyeji wa mchezo inahitaji kumiliki mpira kwa kiasi kikubwa ili iweze kushinda na isipofanya hivyo lazima timu iwe kwenye matatizo.

"Manchester United ilitawala katika idara ya kiungo, lakini PSG ilicheza na viungo watano ambao hawakuwa wakipoteza mpira, Man United haikuwa na uwezo wa kupokonya mipira na pindi inapoupoteza ilikuwa ikipoteza kwa haraka kwasababu PSG ilitawala vizuri katika kurudisha mipira", amesema Wenger.

"Unapocheza nyumbani na huwezi kukaa na mpira, ni lazima utakuwa katika matatizo na hicho ndicho kilichotokea katika mchezo wa leo ( jana ), ambapo Man United imeoneka kuwa na udhaifu katika idara ya kiungo ukilinganisha na PSG ambao walikuwa bora", ameongeza.

Manchester United imepoteza mchezo wa kwanza wa hatua ya 16 bora katika uwanja wake wa nyumbani kwa mabao 2-0, ambapo mchezo wa marudio inahitaji kushinda ugenini kwa mabao 3-0 au zaidi ili kujihakikishia nafasi ya kufuzu hatua ya robo fainali.
 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa