Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga hatuna bahati ya kufunga magoli- Kocha Nabi

Jumamosi , 14th Mei , 2022

Kocha mkuu wa klabu ya Yanga SC Nasreddine Nabi amesema kikosi chake kilikosa bahati ya kufunga kwenye michezo mitatu ya Ligi Kuu iliyopita ambayo yote walitoka suluhu. Amesema hayo kuelekea mchezo wao wa Ligi kesho dhidi ya Dodoma Jiji FC utakao chezwa uwanja wa Jamuhuri Saa 10 jioni.

Kocha wa Yanga Nasreddine Nabi

Nabi amesema hayo alipoulizwa swali kuwa amejipangaje kuhakikisha wanashinda mchezo wa kesho baada ya kucheza michezo mitatu mfululizo ilyopita bila kupata ushindi matokeo ambayo yametengeneza hofu miongoni mwa mashabiki kwenye mbio za ubingwa.

“Hatuna shaka, hatuna wasiwasi, tunaamini uwezo wa kwetu tunaamini uwezo wa wachezaji wetu. Kwenye hizo mechi 3 sio kama mpango wetu haukuwa mzuri, ni mechi ambazo tumepata nafasi nyingi za kufunga magoli lakini tulikosa bahati ya kufunga” Amesema Nasreddine Nabi

Timu ya wananchi inaongoza Ligi ikiwa na alama 57 tofauti ya alama 8 dhidi ya Simba walio nafasi ya pili wakiwa na alama 49, timu zote zikiwa zimecheza michezo 23 ikiwa imesalia michezo 7 kabla ya msimu kumalizika.

Lakini pia kuelekea mchezo huu kocha Nabi amethibitisha kuwa watamkosa kiungo wao Yannick Bangala kwenye mchezo huu. Bangala amefiwa na ndugu yake hivyo hatakuwa sehemu ya mchezo wa kesho. Na kocha huyo ametuma salma za pole kwenda kwa mchezaji huyo kwaniaba ya benchi la ufundi na wachezaji wote wa Yanga.A

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali