Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga wafafanua tiketi zao kuingiliana na Simba

Ijumaa , 9th Aug , 2019

Uongozi wa klabu ya Yanga umefafanua juu ya mkanganyiko uliojitokeza katika mchezo wa kilele cha Wiki ya Mwananchi, Agosti 4 ambapo tiketi za mashabiki ziliingiliana na tiketi za mchezo wa watani wao Simba.

Dismas Ten (kulia) na baadhi ya viongozi wengine

Akielezea hilo katika mkutano na wanahabari Makao Makuu ya Yanga hii leo kwa niaba ya Yanga, mwakilishi wa kampuni ya Salecom inayouza tiketi katika Uwanja wa Taifa amesema kuwa waliweka mechi mbili katika mfumo ili kuwawezesha mashabiki wa timu zote kununua tiketi kwa urahisi ambapo muda uliowekwa ulipoisha, tayari mechi iliyofuata ikaanza kuonesha tiketi zake.

"Huu mfumo upo kidigitali kwahiyo mechi ya Yanga tulipewa 'kick-off' ya saa 5 kwa maana ya shughuli kuanza kwahyo huwa tunahesabu masaa mawili kwa mchezo kumalizika ndio maana ilipofika saa 7 mfumo ukaanza kuonesha tiketi za mchezo unaofuata kwa kuwa ulishapima kuwa mchezo wa kwanza umemalizika", amesema.

"Lakini kwa kile kipande kidogo kilichoonesha tiketi za mchezo unaofuata, ambapo baada ya kugundua tukarekebisha na mapato yaliyoingia katika mchezo huo yakarudhishwa", ameongeza.

Aidha Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga, Dismas Ten amesema kuwa klabu hiyo imejiandaa vya kutosha kuelekea mchezo wa Klabu Bingwa Afrika dhidi ya Towship Rollers kesho Jumamosi, huku akiwataka mashabiki kujitokeza kwa wingi uwanjani kama walivyofanya kwenye kilele cha Wiki ya Mwananchi.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa