Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga yagomea usafiri na hoteli Kenya

Jumanne , 17th Jul , 2018

Klabu ya Yanga ambayo inatarajia kucheza mchezo wa kombe la shirikisho dhidi ya Gor Mahia Jumatano hii, imegomea usafiri walioandaliwa pamoja na hoteli mara baada ya kutua nchini humo.

Kikosi cha Yanga msimu uliopita wa ligi kuu 2017/18

Taarifa zinaeleza kuwa klabu hiyo iliandaliwa usafiri wa basi kutoka uwanjani hadi hotelini lakini ikaukataa na badala yake ikakodi usafiri wao na walipofika hotelini waligoma kuingia ndani ya hoteli bila kutoa sababu yoyote kulingana na maelezo ya katibu wa Gor Mahia, Ben Omondi.

“Tabia hii imekuwa ni kawaida kwa klabu za Afrika lakini nataka kuwahakikishia Yanga kuwa sisi hatujawahi na hatutoshiriki katika masuala ya kishirikina hata mara moja", amesema Omondi.

Juhudi za kumtafuta afisa habari wa klabu ya Yanga, Dismas Ten kuzungumzia suala hilo hazikufanikiwa kwani simu yake haikupokelewa mara kadhaa.

Katika michuano ya CECAFA Kagame Cup, Gor Mahia nao waligomea chumba cha kubadilishia nguo ambacho waliandaliwa kabla ya mchezo wa nusu fainali dhidi ya Azam Fc na badala yake walitumia korido kubadilisha nguo huku wakiituhumu Azam Fc kupuliza dawa katika chumba hicho.

Yanga na Gor Mahia zitachuana katika mchezo wa kundi D wa kombe la shirikisho, ambapo Yanga ikishika mkia katika kundi hilo mbele ya kinara USM Alger ya Algeria na Gor Mahia inayokamata nafasi ya pili.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali