Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Zahera anavyowapoteza mashabiki wa Yanga

Jumatano , 15th Mei , 2019

Licha ya ushindi mwembamba wa jana dhidi ya Ruvu Shooting, kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera ameedelea kubebesha mzigo wa lawama kwa waamuzi na Bodi ya Ligi.

Kocha Mwinyi Zahera (katikati) akisalimiana na Mwenyekiti mpya wa Yanga, Dk Mbette Msolla.

Mara kadhaa, Zahera amekaririwa akiwalaumu waamuzi pamoja na uongozi wa Bodi ya Ligi kuwa wanaikandamiza klabu hiyo katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Baada ya kumalizika kwa mchezo huo dhidi ya Ruvu Shooting, na Yanga kuibuka na ushindi mbembamba wa bao 1-0 kupitia kwa Papy Tshishimbi, kocha Zahera amesema, "malalamiko yangu yapo katika pande mbili, kwanza ni kwa upande wa marefa, wapo wanaokuja wakisema kuwa leo Yanga hatoki".

"Namna nyingine ni kwamba kuna mpango katika timu za Simba na Yanga. Sisi tunacheza FA tarehe 6, Azam FC anacheza na sisi tarehe 29, Lipuli na KMC nao wanacheza FA, lakini hakuna mtu ambaye anacheza ligi wakati anatakiwa kucheza nusu fainali ya FA ni Yanga peke yake", ameongeza.

Tuhuma za Zahera za klabu yake kuonewa limekuwa likibebwa kwa nguvu hadi na mashabiki wa klabu hiyo, wakiamini kuwa ubingwa wa msimu huu wataukosa kutokana na figisu za waamuzi na Bodi ya Ligi ambayo wanaituhumu kuipendelea klabu ya Simba.

Mwinyi Zahera amekuwa akionekana kuwa muwazi hadi kupitiliza na wadau wengi wa soka wanakosoa kitendo hicho kwa kuwa kinamharibia taaluma yake kama mwalimu. Wengi wanaamini majukumu yake ni kuzungumzia mafanikio na mapungufu ya kiufundi ya timu yake pamoja na wachezaji wake, badala ya kujihusisha na malalamiko ambayo yanatakiwa kuwasilishwa kwa Bodi ya Ligi kupitia njia sahihi na uongozi wa klabu.

Yanga hivi sasa inaongoza ligi ikiwa na alama 83 baada ya kucheza jumla ya michezo 36, ikifuatiwa na Simba yenye pointi 82 ambayo imecheza michezo 33.

Bonyeza hapa chini kumsikiliza kocha Zahera.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava