Shabiki Ramadhan Mohamed
Shabiki huyo amepewa ofa ya kusafiri na timu hadi Lubumbashi kuishuhudia na kuisapoti timu yake itakapocheza mchezo wa marudiano wa hatua ya robo fainali na TP Mazembe wikiendi hii.
Shabiki huyo Ramadhan Mohamed aliitwa na viongozi wa klabu, wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi na sekretarieti ambapo amehaidiwa kugharamiwa na klabu kwenda Lubumbashi kuangalia mchezo huo wa marudiano.
Shabiki Ramadhan Mohamed ambaye alikuja Dar akitokea Mbeya kwa miguu ili ashuhudie mchezo #CAFCL dhidi ya TP Mazembe, leo amekutana na viongozi, wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi na sekretarieti ambapo amehaidiwa kugharamiwa na klabu kwenda Lubumbashi kuangalia mchezo wa marudiano. pic.twitter.com/d5O1k35Tg7
— Simba Sports Club (@SimbaSCTanzania) April 8, 2019
Katika mchezo wa awali uliofanyika Jijini Dar e salaam wikiendi iliyopita, Simba na TP Mazembe zilitoshana nguvu ya kutofungana bao lolote. Timu itakayoshinda mchezo huo itafuzu hatua ya nusu fainali ya Klabu Bingwa Afrika.