
Radhia akiwa na watoto wake pamoja na baadhi ya wabunge.
Leo Juni 3,2019, Radhia amewasili bungeni jijini Dodoma ambapo bunge limeridhia kila mbunge wa kiume kumchangia shilingi laki moja na kila mbunge wa kike kumchangia shilingi elfu hamsini fedha ambazo zitatumika kumsaidia kujikimu na kuwatunza watoto hao.
Akizungumza Bungeni jijini Dodoma, Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amesema jukumu la utunzaji wa watoto ni la kila jamii, hivyo bunge limeamua kufanya mchango huo kwa wabunge ili kumsaidia mama na watoto huku akiwaasa wanaume kuacha tabia ya kutelekeza familia zao.
Radhia Solomon alijifungua watoto mapacha wanne Januari 8, 2019 katika hospitali ya Muhimbili Dar es salaam, watoto wa kike wawili Faudhia na Fardhia pamoja na wa kiume wawili Suleiman na Aiman ni pacha wanne ambao kila mmoja alikuwa na mfuko wake wa uzazi na gharama ya kuwanunulia maziwa ya kopo ni shilingi elfu 40 kwa siku kwani alipojifungua afya yake haikuwa nzuri kunyonyesha hali iliyosababisha mumewe kushindwa kumudu gharama na kuwatelekeza