Jumanne , 13th Oct , 2020

Wakazi wa eneo la Mkwajuni Kinondoni jijini, Dar es Salaam, wameiomba serikali kujenga daraja katika Barabara hiyo kutokana na adha inayojitokeza wakati wa mvua ambayo hupelekea barabara kufungwa kutokana na kushindwa kupitika kwa urahisi.

Barabara ya Mkwajuni ikiwa imejaa maji

Wakizungumza na EATV, wakazi hao wamesema kuwa hali sio shwari kwani hali hiyo imekuwa ikijirudia tangu miaka ya 1980, hivyo kuiomba serikali kumaliza kero hiyo.

Kwa upande wao madereva wameeleza kuwa, hali hiyo inapelekea uharibifu wa vyombo vya moto wanavyoendesha lakini wakati mwingine kuhatarisha hata maisha yao kutokana na hatari ya kuvuka maji hayo.

“Ninapopita hapo kuna mawili, nipite salama au chombo changu kizimike katikati ya maji, tunaomba watusaidie kumaliza hii kero” amesema mmoja wa madereva.