
Mchezo wa Juventus dhidi ya Barcelona
Mahasimu hawa wa soka la Ulaya watachuana Jumatano hii, wachezaji wa Barcelona walifungua hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa kwa ushindi mnono wa 5-1 dhidi ya Ferencvaros kutoka Hungary. Matokeo ambayo yanawapa nafasi vijana wa Catalan kuwa miongoni mwa timu zinazopigiwa upatu kubeba taji msimu huu.
Juventus waliwafunga Dynamo Kiev 2-0, mchezo ambao wengi walitegemea ushindi kwa “Kibibi Kizee cha Turin” ambaye pia alitawala mchezo kuanzia mwanzo na Alvaro Morata akahakikisha ushindi unapatikana kwa kufunga magoli yote mawili.
Mchezo wa mwisho kuwakutanisha miamba hii ulichezwa 2017 ambapo Barcelona waliibuka washindi. Kutokana na ukweli kwamba timu zote zimebadilika sana tangu mwaka ule, inakuwa ngumu kutabiri matokeo ya mchezo huu. Kwa upekee wa mchezo huu, wataalamu wa Meridan wameweka odds sawa.
Japokuwa, kwa faida ya kucheza kwenye uwanja wa nyumbani, wengi wanaweza kuwapa nafasi Juventus lakini pia ni muhimu kukumbuka wataikosa huduma ya mchezaji wao nyota, Cristiano Ronaldo ambaye ameshafanyiwa vipimo vya COVID-19 mara 2 na matokeo kuwa ni chanya mara zote.
Ulimwengu wa soka ulishajiandaa kushuhudia upinzani mpya kati ya Cristiano Ronaldo na Lionel Messi ambao ni wachezaji bora duniani kwa karne ya 21 na hili halitotokea kutokana na kumkosa Cristiano Ronaldo kwa upande wa Juventus.
Pamoja na mchezo huu, kunamichezo mingine 7 inatakayochezwa katika mzunguko wa 2 wa Ligi ya Mabingwa, unaweza kujionea odds za michezo hiyo kwa kubofya hapa.
Jisajili na Meridiabet hapa na furaha yako itaanzia hapo. Pakua App ya Meridianbet kwenye simu yako na uanze kubashiri kwa uhuru nyumbani kwako. Pia, unaweza kuweka pesa kwenye akaunti yako kupitia KwikPay, M-PESA au Airtel Money. Kumbuka, daima hauwezi kupoteza tiketi yako ya kwanza ukiwa na Meridianbet, tuna Bonasi ya 100% inakusubiri.
Meridian - Nyumba yenye odds bora na bonasi kubwa