Picha ya aliyekuwa msanii wa muziki wa dansi Waziri Sonyo
Akitoa taarifa za msiba huo kupitia EATV & EA Radio Digital, mchambuzi wa muziki Rajab Zomboko ameeleza kuwa
"Ni kweli amefariki jana, ametoka kuangalia mpira wa Simba alivyofika nyumbani kwake presha ikampanda na wakajaribu kumpepea lakini imeshindikana, msiba upo nyumbani kwake Kibaha Mailimoja, kuhusu mazishi nimeongea na ndugu zake wameniambia watanijulisha"
EATV & EA Radio Digital inatoa pole kwa ndugu jamaa na marafiki wote walioguswa na msiba huu pia wapenzi wa muziki wa Dansi hapa nchini.