
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
Kauli hiyo ameitoa hii leo Chato, Geita, wakati wa kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru, ambapo imebainika kwamba kuna jumla ya miradi ya bilioni 15.3 ambayo imekataliwa na Mwenge huo kwa kuwa haikukidhi viwango vinavyotakiwa.
"Niwatake viongozi wa maeneo, tunapozima Mwenge mwakani idadi ya miradi yenye dosari ipungue sana, na kwa ile mikoa ambayo bado itajitokeza ina miradi yenye dosari tutaelewano wakati huo, hili ni onyo kwa wakuu wa mikoa na wialaya na wakurugenzi," amesema Rais Samia