
Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera, Awadhi Haji
Kamanda wa polisi mkoani Kagera Awadhi Haji, amesema kuwa mauaji hayo yalitokea Desemba 03 mwaka huu, na wote wamekiri kuhusika na mauaji hayo kwa madai ya kwamba marehemu aliwaua ndugu zao kwa njia za kishirikina.
Amesema kuwa baada ya mahojiano ya kina watu hao walisema walimuua mama huyo kwa sababu kuna vifo vya watu wawili vilitokea katika familia zao, na walipokwenda kwa mganga wa kienyeji waliambiwa kuwa Stella ndiye anahusika na vifo hivyo, na kisha kuweka mipango ya kumuua.