Moja ya kaburi lililobomolewa
Kauli hiyo ameitoa wakati wa zoezi la usafi lililofanyika katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo ikiwemo kwenye makaburi ya wilaya ambayo mengine yamebomolewa na watu wasiojulikana.
Kwa mujibu wa Mkuu wa wilaya hiyo amesema kuwa, hadi sasa watu watatu wanashikiliwa kwa tuhuma za kubomoa makaburi hayo na kuiba misalaba pamoja na baadhi ya viungo vya miili iliyozikwa hapo na kwamba uchunguzi utakapokamilika watafikishwa mahakamani.


