Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt.Mwigulu Nchemba
Dkt. Nchemba ametoa rai hiyo mkoani Singida aliposhiriki katika Jubilee ya miaka 50 ya Jimbo Katoliki Singida na kusema Rais Samia ana dhamira ya dhati ya kuwaletea maendeleo wananchi wake, hivyo ni vema kumuombea ili yale aliyodhamiria kwa ajili ya nchi yaweze kutimia.
Aidha amesema kuwa taasisi za dini zina mchango mkubwa katika kuchochea maendeleo ya jamii katika sekta mbalimbali za maendeleo zikiwemo za afya, maji na elimu hususani maeneo ya pembezoni.