Jumatatu , 22nd Aug , 2022

Mkuu wa shule ya Sekondari Faraja pamoja na Mhasibu wa shule hiyo wamefikishwa mbele ya mahakama kuu ya Zanzibar Tunguu kwa tuhuma ya kujipatia fedha zaidi ya milioni 50  kwa njia ya udanganyifu fedha ambazo ni za serikali 

Akitoa taarifa za kufikishwa mahakamani watuhumiwa hao Kaimu Mkurugenzi Mkuu mamlaka ya kuzuiya rushwa na uhujumu uchumi  Zanzibar (ZAECA) Makame Khamis Hassan  kwa kushirikiana na ofisi mkurugenzi wa mashtaka DPP amesema fedha hizo ni  fedha za mradi wa uimarishaji wa mazingira ya kujifunzia wanafunzi Zanzibar (ZISP)

Aidha makame amesema mamlaka imewasilisha kwa DPP jumla ya majalada 12 yaayohusiana na tuhuma mbali mbali za rushwa na uhujumi uchumi kwa hatua zaidi