Jumatatu , 19th Sep , 2022

Watu milioni tisa wametakiwa kuondoka kwenye nyumba zao wakati huu ambao Japan inapitia janga kubwa la kimbunga kikali ambacho kimetajwa kama janga kubwa kuwahi kutokea nchini humo

. Kimbunga Nanmadol tayari kimeshaua watu wawili mpaka sasa na kujeruhi watu takribani 90.

Kimbunga hicho kimepiga kisiwa cha Kyushu siku ya jana na mamlaka za hali ya hewan nchini humo zinasema kwamba kimbunga hicho kitaendelea katika visiwa vya  Honshu ndani ya siku chache zijazo.

Makumi ya watu walitumia siku ya jana kujihifadhi kwenye makazi ya  dharura  ,huku nyumba takribani 350,000 zikikosa umeme.

Usafri na bisahara vimeathiriwa vibaya huku kukiwa na mafuriko na mmomonyoko wa udongo.  Kimbunga Nanmadol kimeleta upepo wenye ksi ya kilomita  234 kwa saa huku baadhi ya maeneo yakipigwa  na mvua zenye ujazo wa   milimita   kwa saa 24.