Alhamisi , 20th Oct , 2022

Mtawala wa kijeshi nchini Chad , Mahamat Idriss Déby, ametangaza hali ya dharura kutokana na mafuriko mabaya kuathiri zaidi ya watu milioni moja nchini humo.  

Katika hotuba yake aliyoitoa kwa njia ya Televisheni, amesema kwamba mvua kali imepiga theluthi ya nchi hiyo kwa karibia kilomita za mraba 5,000 ambazo ni zaidi ya maili 1, na kuua maelfu ya mifugo.  

Mafurriko nchini Chad sio jambo lakawaida sana wakati mvua zinaponyesha, lakini mwaka huu mvua kubwa zimeleta mafuriko makubwa kuwahi kutokea.

Chad ni nchi masikini duniani kwa mujibu wa takwimu za umoja wa mataifa