Jumatano , 26th Oct , 2022

Dereva bodaboda Bakari Yasini (18) mkazi wa Kibaya wilayani Kiteto Mkoani Manyara aliyetoweka siku 6 zilizopita baada ya kukodishwa na mteja, leo Oktoba 26/2022 amekutwa amefariki katika eneo la Lengati Katabya Njoro

Dereva huyo alikodishwa na mtu ambaye hajafahamika tangu Oktoba 21.2022 saa tatu na nusu usiku.

Katika hatua lingine Kamanda wa Polisi Kiteto George Katabazi amethibitisha kupatikana kwa kijana huyo akia amefariki

Aidha Kamanda Katabazi ameeleza kuwa mtu mmoja amefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kujeruhi ng'ombe 4 kwa risasi