Matapeli waanza kuwarubuni walimu ajira mpya 6,000
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe amesema amepata taarifa kuwa wapo watu ambao wamekuwa wakiwatapeli fedha baadhi ya walimu wanaotaka kuomba ajira kwa kuwataka watoe pesa ili wapate ajira.