Mtoto wa miaka mitano abakwa Kagera
Mtoto wa kike mwenye umri wa miaka mitano mkazi wa kijiji Katuruka kata Kanyangereko Bukoba Vijijini ambaye jina lake limehifadhiwa, anaendelea kuteswa na tatizo la kutokwa na mkojo muda wote, alilolipata baada ya kubakwa na mtu anayetajwa kuwa ndugu wa karibu wa mama mzazi wa mtoto huyo.