Simba yainusa robo fainali klabu bingwa Afrika
Wawakilishi wa Tanzania kwenye michuano ya klabu bingwa barani Afrika, klabu ya Simba imeibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Al-Merrrik ya Sudan kwenye mchezo wa mzunguko wa pili wa makundi wa michuano hiyo na kuhitaji alama moja tu ili kutinga hatua inayofuata ya robo fainali.