Bartomeu aachiwa kwa dhamana
Rais wa zamani wa Barcelona, Jose Bartomeu ameachiwa kwa dhamana na mahakama nchini Hispania baada ya jana kushikiliwa na polisi kutokana na tuhuma za kutoa rushwa kwa moja ya kampuni ya mawasiliano kuwachafua baadhi ya nyota wa zamani na wa sasa wa timu hiyo.