Waumini waangukiwa na kanisa, polisi yataja chanzo
Waumini 18 wa Kanisa la Free Pentekoste, lililopo Kijiji cha Kamsisi Kata ya Kamsisi wilaya ya Mlele mkoani Katavi, wakiwamo watoto na watu wazima wamejeruhiwa baada ya kuangukiwa na ukuta wa kanisa hilo wakati ibada ikiendelea, kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha mkoani humo.