Yusuph Mhilu nyota wa Kagera Sugar asiyeimbwa
Mshambuliaji wa Kagera Sugar, Yusuph Mhilu aliendeleza kasi ya kucheka na nyavu msimu huu ambapo jana alifunga bao lake la tatu katika mechi tatu alizocheza licha ya timu yake kupoteza mbele ya Namungo kwa bao 2-1 katika mchezo wa raundi ya tatu ligi kuu ya Tanzania bara.