Cedric Kaze apewa miaka miwili na Yanga
Klabu ya soka ya Yanga imeingia mkataba wa miaka miwili na kocha wao mpya raia wa Burundi Cedric Kaze, ambaye ametua nchini usiku wa kuamkia leo Oktoba 16, 2020. Kaze anachukua nafasi ya Zlatko Krmpotic, ambaye alitimuliwa hivi karibuni baada ya kuifundisha timu kwa siku 37 pekee.