Cedric Kaze apewa miaka miwili na Yanga

Kocha Cedric Kaze (Kulia), akisaini mkataba wa miaka miwili kukinoa kikosi cha Yanga, Pembeni yake (Kushoto) ni Mwenyekiti Dokta Mshindo Msola.

Klabu ya soka ya Yanga imeingia mkataba wa miaka miwili na kocha wao mpya raia wa Burundi Cedric Kaze, ambaye ametua nchini usiku wa kuamkia leo Oktoba 16, 2020. Kaze anachukua nafasi ya Zlatko Krmpotic, ambaye alitimuliwa hivi karibuni baada ya kuifundisha timu kwa siku 37 pekee.

Pages

Subscribe to East Africa Television RSS