"Upitishaji nguzo za umeme haujazuiliwa"- Masanja
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja amesema serikali kupitia Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) haijazuia vibali vya kukamilisha miradi ya kimkakati ya kupeleka umeme vijijini kwa kupitisha nguzo za umeme katika hifadhi za misitu nchini.