Shangazi ataka kuua mtoto kwa kumnyonga
Mtoto wa kike mwenye umri wa miaka saba mkazi wa mtaa wa Mission, Kata ya Pamba wilayani Nyamagana jijini Mwanza, amenusurika kifo baada ya kunyongwa na shangazi yake Elizabeth Bagwisa kwa madai kuwa alikuwa anacheza nyumba ya jirani ambapo shangazi yake huyo alimkataza.