Wenye guest kulipa kodi ya kitanda
Wafanyabiashara wa nyumba za kulala wageni mkoani Geita, wameiomba serikali kupitia upya mapendekezo ya kodi mpya ya asilimia 1 ya kitanda wanayotakiwa kulipa kila mwezi kwani kodi zinazidi kuwa nyingi hali inayoweza kupelekea kufunga biashara zao.