Mtoto aliyeibiwa Bukoba apatikana Dodoma
Jeshi la Polisi mkoani Kagera linawashikilia watu watano kwa tuhuma za kuhusika na wizi wa mtoto mchanga mwenye umri wa mwezi mmoja Benita Beneti, ambaye aliibwa Desemba 01 mwaka huu katika mtaa wa Migera, Kata ya Nshambya katika Manispaa ya Bukoba, na kupatikana Desemba 08 mkoani Dodoma.