Wananchi Kagera walia na uchafu
Baadhi ya wakazi wa kata za Bilele na Bakoba katika manispaa ya Bukoba mkoani Kagera, wameiomba serikali kuwachukulia hatua kali wananchi ambao wanazalisha taka na kuzitupa katika mto Kanoni, maana kufanya hivyo wanahatarisha afya na usalama wao.