Katibu mkuu kiongozi balozi Ombeni Sefue. Ofisi yake imekana kuwa na taarifa ya tuhuma za kuingilia mambo ya ndani zinazomkabili balozi wa Uingereza nchini Bi. Dianna Melrose.
Ikulu jijini Dar es Salaam nchini Tanzania, imekana kuwa na taarifa za madai ya uchochezi unaofanywa na balozi wa Uingereza hapa nchini Bi. Dianna Melrose, kama zilivyotolewa na wizara ya nishati na madini.