Mkanda wa Nyilawila na Mbelwa hadharani.

Anthony Luta (katikati) akiwa na mkanda utakaopiganiwa na Kalama Nyilawila(kushoto) na Said Mbelwa(kulia)

Waandaaji wa pambano la masumbwi ya kuwania ubingwa wa kimataifa wa UBO uzito wa Super Middle kati ya Kalama Nyilawila na Said Mbelwa, wamesema maadalizi yamekwisha kamilika kwa kiasi kikubwa na kilichobaki ni masuala madogo madogo ambayo yatakamilika kadri siku zinavyosogea.

Akiozungumza EATV wakati akitambulisha mkanda utakaopiganiwa, katibu mkuu wa PST ambao ndiyo wasimamizi wa pambano hilo bwana Anthony Luta amesema pambano hilo litakutanisha mabondia wenye sifa tofauti.

Pages

Subscribe to East Africa Television RSS