Swahili Fashion Week 2013
Swahili Fashion Week ni tamasha linayofanyika kila mwaka Afrika Mashariki ambapo wanamitindo wanapata fursa ya kuonyesha mitindo mbalimbali ya mavazi.
Katika tamasha hili linalodhaminiwa na East Africa television toka mwaka 2008, linaendesha mashindano ya mitindo mbalimbali na ubunifu katika nyanja tofauti za kijamii.
Tamasha hili lina vipengele mbalimbali kama uvaaji wa mitindo na hata utangazaji wa mitindo.