Mwanafunzi ajeruhiwa kwa kuchomwa kisu kisa 4000
Mwanafunzi Jackson Stephen wa kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Kagemu iliyoko katika manispaa ya Bukoba, amelazwa katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Kagera, baada ya kujeruhiwa kwa kuchomwa kisu mara mbili katika paja lake la mguu wa kulia na mwanafunzi mwenzie akidaiwa 4000.