Rais Paul Kagame wa Rwanda, akiwa na mwenyeji wake Rais Jakaya Mrisho Kikwete wa Tanzania, wakati kiongozi huyo alipowasili kwa ajili ya mkutano wa wakuu wa nchi zinazounda ukanda wa maendeleo wa kati jijini Dar es Salaam leo.
Wauguzi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakimpokea Dada Neema Mwita Wambura (32) na kuanza mara moja kumfanyia tena uchunguzi wa afya yake katika majeraha aliyoyapata mara baada ya kumwagiwa uji wa moto uliokuwa ukichemka jikoni kitendo kilichofanywa na mume wake.