Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Upanuzi kiwanda suluhu ya soko la miwa Kilombero

Jumatatu , 7th Jun , 2021

Waziri wa Viwanda na Biashara, Prof. Kitila Mkumbo, amesema suluhu ya kudumu ya miwa ya wakulima wa Kilombero ni upanuzi wa kiwanda cha Kiwanda cha Sukari cha Ilovo, ambacho kitawasaidia kuuza zaidi miwa yao.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Prof. Kitila Mkumbo,

Prof. Mkumbo amebainisha hayo katika kipindi cha maswali na majibu Bungeni, leo Juni 07 ambapo amesema upanuzi huo utaongeza uzalishaji wa sukari katika Kiwanda hicho kutoka tani 127,000 kwa mwaka hadi tani 271,000 kwa mwaka ikiwa ni ongezeko la tani 144,000.

“Suluhu ya kudumu ya miwa ya wakulima wa miwa kilombero ni upanuzi wa kiwanda hiki kwani wakulima watauza zaidi miwa yao kwa sababu kiwanda kitakuwa na uwezo wakuchukua zaidi ya mara tatu ya miwa wanaochukua sasa hivi,” amesema Prof. Mkumbo.

Aidha, Prof. Mkumbo ameahidi kufuatilia uhujumu wa wakulima wa miwa uliobainishwa na Mbunge wa Jimbo la Mikumi Dennis Londo akiitaka kujua tamko la serikali juu ya wanaotaka (kiwanda) kuhujumu wakulima wa miwa na Watanzania wanaoshirikiana na wawekezaji katika hilo.

“Tamko la serikali kuhusu wawekezaji wa viwanda Serikali inataka wawekezaji wote nchini kufanya shughuli zao kwa kuzingaia sheria na kama kuna hujuma kama alivyoeleza Mheshimiwa mbunge tutafuatilia,“ amesema Waziri Kitila Mkumbo.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala