Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wazabuni wa Dawa watakiwa kuwa wazalendo

Jumatano , 21st Apr , 2021

Wazabuni wa Dawa, Vifaa Tiba na Vitendanishi vya maabara nchini wametakiwa kuzingatia maadili ya biashara ya dawa kwa kuweka mbele suala la uzalendo na ubora ili Serikali kupitia Bohari ya Dawa (MSD) iendelee kuimarisha uhusiano wa manunuzi uliopo baina yao.

Katibu Mkuu, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto-Idara Kuu Afya, Prof. Abel Makubi wakati akizungumza na wazabuni wa Dawa, Vifaa Tiba na Vitendanishi vya maabara nchini.

Hayo yameelezwa Jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto-Idara Kuu Afya, Prof. Abel Makubi wakati akizungumza na wazabuni hao ambao wanauza na wanasambaza bidhaa hizo kwenda MSD.

Prof. Makubi amesema kuwa moja ya vipaumbele vya Serikali ni kuhakikisha upatikanaji wa dawa za kutosha na zenye viwango zinazopelekwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ili wananchi wapate huduma bora za afya wakati wote na popote.

Serikali imejipanga vizuri kuhakikisha upatikanaji wa dawa, vifaa na vitendanishi vya maabara kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini zinaimarika,hivyo mnatakiwa kuweka mbele uzalendo , uaminifu , uhalisia wa bei na mzalishe bidhaa zenye ubora ili kukidhi matakwa ya serikali na kupunguza gharama za matibabu Kwa wananchi na hata kwa mifuko yetu ya Bima", amesisitiza Prof. Makubi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa MSD Meja Jenerali Dkt. Gabriel Saul Mhidze amewashukuru wazabuni kuendelea kuiamini MSD na kuipa huduma pamoja na ushauri ambao wamekuwa wakimpatia ili kuboresha huduma ya upatikanaji wa dawa nchini.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi