Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kwanini hofu imetanda kuhusu ndege za Boeing 737?

Jumatatu , 11th Mar , 2019

Ikiwa ni masaa machache tu tangu ndege inayomilikiwa na shirika la ndege la Ethiopia aina ya Boeing 737 Max 8, kuanguka na kuua watu wote 157 walikuwemo, imebainika kuwa ndege ya aina hiyo ilianguka miezi mitano iliyopita na kuua watu wote 189 waliokuwemo.

Ndege hiyo ambayo ilikuwa inamilikiwa na shirika la ndege la Lion nchini Indonesia, ilianguka Oktoba 29, 2018 na kuua watu wote 189 waliokuwemo, na kupelekea kufananisha na ajali ya Boeing 737 Max 8 ya Ethiopia iliyotokea Machi 10, 2019

Ajali ya ndege ya Lion ilitokea dakika 13 tu baada ya kupaa kutoka katika Uwanja wa Ndege wa Jakarta Indonesia, wakati ajali ya ndege ya Ethiopia imetokea dakika 6 baada ya kutoka Uwanja wa Ndege wa Adis Ababa.

Ndege ya Lioni ambayo ni Boeing 737 Max 8 Ndege ya Lion ilipoanguka baharini na kuua watu 189

Usichokijua kuhusu Boeing 737 Max 8

Boeing 737 MAX ni ndege ya biashara inayotengenzwa na kampuni ya Boeing ya Marekani, ambao pia ni watengenezaji wa ndege ya Boeing 787 Dreamliner, iliyonunuliwa na Tanzania hivi karibuni.

Ndege ya Boeing MAX 8 ilianza kuingia sokoni kwa mara ya kwanza Mei 16, 2017, baada ya kununuliwa na Shirika hilo la Ndege la Lion linalofanya safari za ndani nchini Indonesia.

Ndege hizo ziliendelea kuuzwa kwa nchi mbalimbali, ambapo Ethiopa ilinunua yakwake mwaka 2018, na kuwa nchi ya kwanza Afrika kununua aina hiyo ya ndege.

Baada ya ajali hizi mbili za karibuni zilizotokea, utengenezaji wa ndege hizo umeanza kuzua wasiwasi miongoni mwa mashirika mengi ya anga duniani, ambapo Mamlaka ya Udhibiti wa Safari za Anga ya China imetangaza kusitisha kutumia ndege hizo.

Vile vile shirika la ndege la Ethiopia limetangaza kusitihsa kutumia ndege zake zote aina ya Boeing, ili kuchukua tahadhari zaidi baada ya ajali kutokea, ambayo mpaka sasa haijajulikana imesababishwa na nini.

 

HABARI ZAIDI

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya