Jumatatu , 27th Mar , 2023

Watuhumiwa 17 wa matukio ya utekaji magari  na kunyang'anya fedha  kwa kutumia silaha wamekatwa mkoani Njombe baada ya msako mkali  ulioshirikisha   Makamanda wa Jeshi la Polisi wa Mikoa Mitatu ya Nyanda za Juu Kusini, Njombe ,Iringa na Mbeya

Msako huo umefanyika baada ya kuibuka matukio ya kihalifu ambayo ni pamoja na utekaji magari na kupora fedha za madereva na abiria.

Tume ya kudhibiti matukio hayo iliundwa kwa kujumuisha mikoa mitano ya Nyanda za Juu Kusini  kwa kujumlisha mkoa wa Njombe,Ruvuma,Iringa ,Songwe na Mbeya  ambapo  watuhumiwa 69 wa matukio mbalimbali ya uhalifu wamekatwa na kufikisha jumla ya watuhumiwa 87  baada ya msako huo.