Jumanne , 13th Mei , 2025

Jumla ya watu 10 wamejeruhiwa baada ya treni ya abiria maarufu kama treni ya Mwakyembe inayofanya safari zake kati ya Kariakoo na Pugu jijini Dar es Salaam, kupata ajali baada ya mabehewa yake matatu kuacha njia.

Treni iliyopata ajali

Ajali hiyo imetokea leo Mei 13, 2025, majira ya saa 11:00 jioni eneo la Kamata ikielekea Machinga Complex uelekeo wa Pugu.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Amana, amekiri kupokea majeruhi 10 waliotokana na ajali hiyo kati yao nane ni wanawake na wawili ni wanaume.