Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Alichokisema Mdee kuhusu nani aliyepeleka majina

Jumanne , 1st Dec , 2020

Mbunge wa viti maalum kupitia CHADEMA,Halima Mdee, amesema kuwa hawezi kusema ni nani aliyepeleka majina yao Bungeni na wala ni kwanini waliapa, kwa kuwa hataki kuweka mambo hayo hadharani na badala yake ataenda kuyazungumza ndani na viongozi wa chama chake.

Halima Mdee na wenzake wakati wakizungumza na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam.

Kauli hiyo ameitoa hii leo Disemba 1, 2020, wakati wa mkutano wake na wabunge wenzake walioapishwa hivi karibuni, ambapo amesema kuwa yeye na wenzake kuanzia sasa ni wana CHADEMA wa hiyari na wala hawana mpango wa kuondoka ndani ya chama hicho kwa sababu wametoka nacho mbali.

"Kamati kuu imefanya uamuzi wake, tumesema tunaenda kukata rufaa baraza kuu, hizi hoja mbili ya kwanini tumeenda kuapa, au nani amepeleka majina ndiyo msingi wa rufaa zetu, siwezi kujadili hapa content , ndiyo maana nilisema kuna maswali nitayajibu na sitoyajibu tutaliongea ndani ya chama kwa sababu kila mtu ameshasema la kwake na hili ndiyo msingi mkuu wa kesi yetu", amesema Halima Mdee.

Aidha Mdee ameongeza kuwa, "Mimi sina dhamira ya kuondoka CHADEMA na hapa kila mmoja ameijenga CHADEMA kwa jasho na damu yake pamoja na changamoto tunazopitia maana hii wiki moja ilikuwa ya makashikashi kweli, niwahakikishie Halima mnayemfahamu miaka yote ndiyo yuleyule".

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea