Katibu Mkuu wa CCM Daniel Chongolo
Kauli hiyo ameitoa hii leo Juni 25, 2023, jijini Dodoma, wakati akihitimisha ziara yake mkoani humo iliyokuwa na lengo la kuimarisha chama, kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali pamoja na kuangalia uhai wa chama hicho.
"Hakuna mgogoro wa ardhi unaotoka mbinguni ukashuka na kuwakuta watu wakiwa salama na kuwa mgogoro, mgogoro wowote wa ardhi ujue yupo mtu anayeutengeneza, lazima kipo chanzo husika, Dodoma ni Makao Makuu ya nchi hatuwezi kupaacha kuwa sehemu ya migogoro," amesema Chongolo
Aidha Chongolo ameongeza kuwa, "Lazima tuweke mipango ya kutatua migogoro Dodoma, na sisi tutaingia katikati kufuatilia hatua kwa hatua kuona ni namna gani tunaenda kumaliza migogoro hii, tujue ni nani aliyeisababisha na yuko wapi sasa, na waliopata madhara hayo wanafanyiwa nini ili kuondokana na madhira hayo".