Ijumaa , 1st Oct , 2021

Jeshi la Polisi mkoa wa Simiyu, linamshikilia mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 49, kwa tuhuma za kumbaka mtoto wake wa kambo mwenye umri wa miaka sita kwa kile kilichoelezwa kuwa ni tamaa za kimapenzi.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Simiyu, ACP Richard Abwao

Taarifa hiyo imetolewa leo Oktoba Mosi, 2021, na Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Simiyu, ACP Richard Abwao, ambapo amesema tukio hilo limetokea Septemba 22, mwaka huu majira ya saa 3:00 usiku Kitongoji cha Majengo, Kata ya Dutwa wilayani Bariadi.

Video hapa chini